Showing posts with label WASANII. Show all posts
Showing posts with label WASANII. Show all posts

Profesa Jay akumbuka msoto wa Maisha....Asimulia Alivyokuwa Anakunywa Maji ya Chooni na Kupanda Malori

Nguli wa muziki wa Bongo Fleva ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Mikumi, Joseph ‘Profesa Jay’ Haule, amekumbuka msoto aliokutana nao wakati anatafuta kutoka kimuziki miaka ya 1990 akiwa na Hard Blasters Crew (HBC).

Akifunguka kupitia The Playlist ya Times FM, rapa huyo mkongwe aliyechonga barabara kwa wasanii wengi wa rap nchini, amesema kuwa wakati wanaandaa albam zao na HBC, hawakuwa na kitu mfukoni kiasi cha kufikia hatua ya kunywa maji ya bomba lililokuwa chooni ili waendelee kufanya kazi yao studio.

“Nakumbuka wakati huo tunarekodi, unaenda kunywa maji chooni hivi… kwenye bomba liliko chooni unakula na mihogo yako ili uweze ku -buy time ya kuendelea kuwa studio siku nzima. Kwamba hakuna hata pesa ya kula chips mzee,” Profesa alifunguka.

Mkali huyo wa rap mwenye majina mengi ya kupewa kwa kuwa mbabe wa kurap, alieleza kuwa wakati wamepata nafasi ya kurekodi albam yao kama HBC, kuna wakati akiwa anafanya kazi Tanga, ilimlazimu kupanda malori ya mizigo usiku ili arejee kazini Jumapili usiku, kwani muda wa usiku aliokuwa akimaliza kurekodi jijini Dar es Salaam, magari ya abiria hayakuwepo.

Katika hatua nyingine, Profesa Jay alieleza tukio la kurekodi wimbo wake wa ‘Jina Langu’ katika studio za Bongo Records chini ya mtayarishaji nguli, P-Funk Majani. Alisema alimshangaza Majani kwani alikuwa akisikia mara kadhaa mdundo wa wimbo huo, ndipo alipomuomba mtayarishaji huyo aingize sauti.

Alisema baada ya kuwekewa mdundo, alipita na mashairi yote matatu bila kukwama, kitu ambacho kilimshangaza Majani pamoja na ukubwa wa mashairi yaliyowekwa ndani.

Profesa amewashauri wasanii wa Tanzania kuendelea kuandika vitu ambavyo vinagusa jamii na kuitangaza Tanzania kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.

Hivi karibuni, aliachia wimbo wake ‘Pagamisa’ akiwa na mtayarishaji wa muziki, Mr. T-Touch.
Read More

Bata la Zari Dubai lawachanganya wengi



 DAR ES SALAAM: Wakati suala la mzazi mwenzake Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kutanua pande za Dubai likidaiwa kuwezeshwa na kigogo mmoja, imebainika tofauti na maneno ya watu mitandaoni.

Kwa takriban wiki moja na zaidi, Zari ameonekana Dubai akiwa na wanaye wakubwa watatu, wakila bata katika viunga mbalimbali vya kuponda raha hali iliyofanya watu wengi kutoa maoni yao mitandaoni.
Kuna baadhi ya watu walimsifia kwa kueleza kuwa anachokifanya ni sahihi kwani anao uwezo wa kifedha hivyo kula bata si tatizo, tofauti na wanawake wenzake waliowahi kutoka na Diamond, Wema Sepetu na Hamisa Mobeto.
Kuna wengine walimponda kwa madai kuwa fedha hizo anazotumia, si zake bali kuna kigogo anayemwezesha hivyo asijishebedue na kuwarusha roho kina Wema na Mobeto.
Risasi Jumamosi lilifanikiwa kuzungumza na mtu wa karibu na Zari ambaye aliomba hifadhi ya jina na kubainisha, licha ya Zari kuwa na fedha zake lakini nyuma ya safari yake hiyo, yupo mdhamini anayemwezesha.Alisema, safari hiyo Zari amedhaminiwa na kampuni moja (jina kapuni) ambaye ndiye anayempa jeuri hiyo.
“Watu hawajui tu. Nimeona wanasema mengi sana mitandaoni, ooh sijui kuna kigogo sijui Zari hana pesa ya kukaa Hoteli ya Dusit Marina pale Dubai, kwanza watambue Zari ana fedha.
“Mtu anamiliki mashule, ana maduka Afrika Kusini atashindwa kulipia hoteli shilingi milioni tano kwa siku? (Chumba cha hoteli hiyo gharama yake kwa siku ni kati ya shilingi laki 5 na milioni moja na ushee),” alisema mtu huyo wa karibu na Zari.
Kama hiyo haitoshi, mtu huyo aliweka bayana kuwa licha ya kujimudu kifedha, safari hiyo Zari alidhaminiwa na ndio maana hata picha alizoposti kwenye mtandao wa Instagram, amewataja wadhamini.
Risasi Jumamosi liliingia kwenye kurasa mbalimbali katika mtandao wa Instagram na kukutana na kampuni hiyo iliyomdhamini Zari.
Hadi tunakwenda mitamboni juzi, imeelezwa kuwa Zari pamoja na wanaye watatu wakubwa pamoja na kijana mwingine, walikuwa bado wapo Dubai wakitumbua maisha.
Read More

Diamond afunguka kuhusu kuvaa msalaba



MWANAMUZIKI kiwango kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, amefunguka kwamba watu wamekuwa wakimdis kutokana na kuvaa kwake cheni yenye msalaba bila kufahamu nini anamaanisha.

Akichonga na Mikito Nusu Nusu, Diamond alifunguka kwamba kwake huwa hachukulii cheni hiyo kama msalaba, bali ni alama ya jumlisha ambaye kwake inamaana kubwa ambayo ni siri yake.
“Cheni ninayovaa na watu kunidisi kwamba ni msalaba kiukweli huwa ninashangaa sana kwa maana watu huzungumza kile ambacho hawakifahamu. Kwangu huo si msalaba, bali ni alama ya jumlisha ambayo ninaona haina tatizo lolote, kwani alama hiyo inamaana kubwa kwangu ambayo itabaki kuwa siri yangu!” alisema Diamond.
Read More

Alichosema Mama Kanumba katika Kanumba Day

Wadau wa tasnia ya filamu na familia ya marehemu Steven Kanumba, leo wanaadhimisha miaka sita tangu kufa kwa msaanii huyo.

Mama yake Flora Mtegoa, amesema yeye kwake msiba huo bado upo kila siku na kudai kila nafsi itaonja mauti.

Mtegoa ameyasema hayo leo Aprili 7 katika makaburi ya Kinondoni ambapo walifanya ibada fupi kwa ajili kumbukumbu hiyo akiwa na baadhi ya wasanii hususani wa kikundi cha Soweto ambao ndio wameisimamia shughuli hiyo kwa mwaka huu.

Amesema pamoja na kujitokeza kwa wasanii wachache ambao waliwahi kufaya kazi na mtoto wake enzi za uhai wake anaamini ni kutokana na wao kuona wameshamaliza msiba, lakini kwake upo kila siku na kamwe hauwezi kufutika mpaka mwisho wa uhai wake.

"Ni kweli idadi ya wasanii maarufu waliokuja hapa ni wachache ukilinganisha na namna Kanumba alivyoishi nao, lakini ndio hivyo huwezi kuwalazimisha na isitoshe wao labda wanaona wamemaliza msiba lakini kwangu bado upo ila ninachowaombea yasije yakawakuta kama haya ndio watajua nini namaanisha,’’ amesema Mama Kanumba.

Wito wake kwa wasanii Mama Kanumba amewashauri kuwa na upendo kauli ambayo Kanumba alikuwa anapenda kuisema enzi za uhai wake.
Read More

Nisha Akana Skendo Ya Kumtongoza Young Dee

Muigizaji wa Bongo movie  Salma Jabu 'Nisha'   anayefanya vizuri hivi sasa na ngoma yake ya Bachela amejibu tuhuma alizotupiwa kuwa ana Mahusiano ya kimapenzi na msanii wa Bongo fleva Young Dee.

Siku ya Alhamis msanii wa Bongo fleva Amber Lulu alitoboa Siri na kusema kuwa kipindi ana Mahusiano ya kimapenzi na Young Dee, mwanadada Nisha alikuwa anamtongoza Young Dee.

Amber Lulu aliweka wazi kuwa jambo hilo lilikuwa la wazi hadi alikuwa ana ushahidi kwani alikamata meseji za wawili hao huku akikiri kuwa Nisha ni fundi wa mapenzi maana alikuwa anampa maneno matamu Young Dee.

Baada ya kutupiwa tuhuma hizo Enews ya EATV ili mtafuta Nisha kwa ajili ya kujibu tuhuma hizo na moja kwa moja alikataa na kusema kuwa hajawahi kuwa na Mahusiano na Young Dee zaidi ya urafiki:

"Mimi sina Mahusiano na Young Dee ila kilichotokea ni kwamba nilikuwa nataka kuingia kwenye muziki hivyo  Young Dee kama msanii wa Bongo fleva alikuwa ananisaidia na lazima niwe karibu na wasanii we zangu.

" Alafu mimi nimemjua Young Dee kabla hata hajawa na Mahusiano na Amber Lulu kwaiyo ni mtu wangu wa karibu na trust me angekuwa mpenzi wangu nisingeweza kuficha maana mimi nikipenda nataka watu wote wajue”.
Read More

Tuzo za Sinema Zetu Zampa Dili Nono Wema Sepetu



MWIGIZAJI bora wa kike katika tasnia ya filamu nchini Tanzania Wema Sepetu amesaini mkataba mnono na Kampuni ya Auguster kwa ajili ya usambazaji wa filamu yake ya Heaven Sent.
Mkataba huo umesainiwa leo katika mkutano uliofanyika ndani ya studio za Azam TV jijini Dar es Salaam, ambapo kampuni hiyo imewakilishwa na Ofisa Uhusiano wake Nembris Soka.

Tukio pia limeshuhudiwa na mwandishi na muongozaji wa filamu hiyo, Neema Ndepanya.
Kwa upande wa Wema amesema tangu kutolewa rasmi kwa filamu hiyo, wapenzi wake wamekuwa wakiipata kupitia ‘Application’ ya Wema Sepetu, na hapakuwa na DVD zozote ambazo zilikuwa zikisambazwa kwa watu.
Amesema kampuni hiyo imeamua kufanya kazi hiyo baada ya filamu hiyo kushinda tuzo mbili katika Tuzo za Kimataifa za Filamu (SZIFF) zilizofanyika Aprili  MOSI, mwaka huu katika Ukumbi wa Mlimani City.
Soka yeye amesema Kampuni ya Auguster wamevutiwa na kiwango cha filamu hiyo na wameona jinsi mashabiki wa filamu nchini walivyo na kiu ya kuitazama filamu hiyo, na ndiyo maana wameamua kuifanya kazi hiyo ya usambazaji ili iwafikie watu.
Read More

Roma akamilisha Usajiri BASATA

Msanii Roma Mkatoliki ametimiza masharti aliyopewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe kumtaka ajisajili Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na kuwa akifanya hivyo atakuwa ametambulika na kuwa huru kufanya kazi.

Roma Mkatoliki jana  April 5, 2018 amekwenda Baraza la Sanaa la Taifa na kujisajili kama ambavyo aliagizwa na viongozi wa serikali na kusema kuanzia leo atakuwa huru kufanya kazi na sasa anarudi rasmi katika muziki.

Mar 1, 2018 Msanii wa muziki wa Hip Hop bongo Roma Mkatoliki alifungiwa kufanya shughuli za muziki kwa muda wa miezi sita kwa kile kilichodaiwa msanii huyo kudharau wito wa BASATA na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. 
Msanii huyo ametumikia kifungo hicho kwa mwezi mmoja na siku tano hivyo kifungo chake kimeisha jana baada ya kujisajili BASATA.

Msanii Roma Mkatoliki ajisajili na kukabidhiwa rasmi cheti cha kutambulika na Baraza la sanaa la Taifa jana April 05 2018, Hii ni baada ya kupewa sharti na Wizara ya Habari ya kujisajili kwanza Basata ili aondolewe adhabu yake ya kufungiwa miezi 6.
Read More

Shilole Achora Tatoo ya Mwisho Yenye Jina la Mumewe

Mwanamuiki wa kike ambae pia ni mjasiriamali, Shiloleh ameonyesha tatoo aliyochora kwenye mwili wake yenye jina la mume wake mpendwa uchebe yenye jina ‘ASHRAF‘  na kusema kuwa hiyo ndio tatoo yake ya mwisho kuichora katika mwili wake.

Katika ukurasa wake wa instagram , Shilole aliandika;“Kwa mara ya kwanza na ya mwisho nimechora tatooooo ya jina la mume wangu Nampendaa sana”

Shilole aliwahi pia kuchora tattoo ya aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda na baadae kuifuta na hii itakuwa tattoo yake ya pili kuichora yenye jina la mwanaume ambae ni mpenzi wake na kuionyesha hadharani..

Read More

Ebitoke ajibu ishu ya kumsaliti Ben Pol na kutembea na Shemeji yake

Mchekeshaji kutoka kundi la Timamu, Ebitoke amejibu tetesi za kutoka kimapenzi na Wyse ambaye ni msanii anayesimamiwa na Ben Pol.

Utakumbuka kuwa Ebitoke na Ben Pol kwa kipindi kirefu sasa wamekuwa wakieleza kuwa wao ni wapenzi hivyo, Wyse ni shemeji yake na Ebitoke.

Mchekeshaji huyo amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote kwani mapenzi yake na Ben Pol bado ni ya moto kabisa na picha zilizotoka wakiwa wana-kiss ni katika kutengeneza video ya Wyse.

“Director alituambia tu-kiss ili kuvaa uhalisia ila kati yangu na Wyse ni urafiki hakuna mapenzi,” Ebitoke ameiambia Bongo5.

Muimbaji Wyse anasimamiwa na Ben Pol na kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Siamini’, pia alishirikishwa na Ben Pol katika wimbo wake uitwao Bado Kidogo.
Read More

Kajala afunguka kuongeza mtoto wa pili na mipango ya mwanae

Msanii wa filamu Bongo, Kajala Masanja amesema hatarajii kabisa kuwa mwanae, Paula ataingia katika tasnia ya burudani nchini.

Muigizaji huyo ameiambia Planet Bongo ya EA Radio mwanae ana mpango wa kuwa mwanasheria na si nje ya hapo.

“Hivi vitu industry, sijui radio, muziki, movie hapana , hayupo interest kabisa yeye kila siku anaseama anataka kuwa mwanasheria, kwa hiyo tunasubiria amalize shule tuwe na mwanasheria mkali,” amesema.

Alipoulizwa kuhusu kuongeza mtoto wa pili, alijibu; “Mungu akijalia atotokea mwingine tu soon,”.
Read More

Diamond, Samatta Waitwa Marekani Kutunukiwa Tuzo

Diamond, Samatta Waitwa Marekani Kutunukiwa Tuzo
Mwanamuziki wa kizazi kipya, Nassib Abdul maarufu Diamond Plutnumz na mwanasoka wa kimataifa, Mbwana Samattapamoja na Watanzania watatu na raia wa Marekani, wameteuliwa kutunukiwa tuzo katika tamasha lililoandaliwa na Watanzania waishio ughaibuni (Diaspora) litakalofanyika Dallas nchini Marekani.

Katika tuzo hizo atapewa  Dk Steve Meyer ambaye ni daktari bingwa katika Hospitali ya Mercy iliyopo jiji la Sioux, Marekani aliyewatibu manusura wa ajali ya wanafunzi wa Lucky Vincent.

Akizungumza na gazeti hili kutoka Dallas jana, mratibu wa tamasha hilo, Ben Kazora alisema wanampa tuzo daktari huyo kwa kutambua mchango wake katika kuokoa maisha ya watoto hao.

“Sote tunatambua namna ajali ilivyokuwa mbaya na ilivyopoteza wapendwa wetu wengi. Dk Meyer na timu yake walifanya kila njia kuokoa maisha ya watoto wale watatu walionusurika,” alisema.


“Tunampa Diamond zaidi kwa kutumia kipaji chake cha muziki kuitangaza nchi kitaifa na kimataifa, vivyo hivyo Samatta kwa kutumia kipaji chake cha kusakata kabumbu kuitangaza Tanzania,” alisema.

Kwa mujibu wa Kazora, mwingine ni mwanariadha John Akhwari ambaye mwaka 1968, alimaliza mbio katika michezo ya Olympic iliyofanyika Mexico City licha ya kuumia mguu.

Naye meya wa Dallas Texas nchini Marekani, Mike Rawlings aliwakaribisha Watanzania hao kushiriki tamasha la Tanzania Day, litakalofanyika jijini humo kwa lengo la kutangaza fursa za biashara na utalii.
Read More

Babu Seya na Papii Kocha Baada ya Kuachiwa Huru Jana Jioni

Mwanamuziki Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ wametoka katika gereza la Ukonga jana jioni  baada ya kusota kwa miaka 13.

Wanamuziki hao ‘baba na mwana’ walitoka katika kifungo cha maisha baada ya kupata msamaha wa Rais John Magufuli  jana Jumamosi Desemba 9, mwaka 2017.

JPM alitoa msamaha kwa baadhi ya wafungwa alipokuwa akihutubia Taifa kusherehea miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara na miongoni mwa waliopata ahueni hiyo ni Babu Seya na Papii Kocha.

“Babu, babu, babu,” zilikuwa ni kelele za mashabiki na ndugu zake waliompokea Babu Seya na Papii Kocha waliokuwa wametoka gerezani wakiwa na magitaa yao mgongoni.

Babu Seya aliyeonekana mtanashati alionekana anapunga mkono wa kulia kama mtu asiyeamini huku Papii Kocha akipunga mkono akionekana kufurahia na kuzungumza na mashabiki.

Walisindikizwa na askari magereza mpaka nje na kulikuwa na foleni kubwa kutokana na tukio hilo.
Read More

Maneno ya Diamond kwa Lulu Michael Baada ya Kuhumiwa Miaka Miwili

Mwanamuziki Diamond Platnumz amesema hukumu ya miaka miwili aliyopewa mwigizaji Elizabeth  Michael maarufu Lulu siyo adhabu bali ni mtihani ambao unalenga kumfanya kuwa imara zaidi.


Amesema mwigizaji huyo ambaye leo Jumatatu Mahakama Kuu imemhukumu kifungo cha miaka miwili jela, amechaguliwa na Mungu kwa kuwa anaamini anao uwezo wa kuhimili mikikimikiki.

Katika mtandao wa Instagram, Diamond anayetamba na wimbo Halleluyah, ameandika:  "Mwenyezi Mungu ameamua kukupa mtihani huu wewe kwa sababu anaamini wewe ni shujaa na imara...pia anaamini wewe ndio msichana pekee unayeweza kuuhimili mtihani huu... hivyo usisononeke, Make him Proud.”

Mbali na Diamond, wasanii wengine wametuma salamu za pole kwa Lulu akiwamo Wema Sepetu, Mboni Masimba, Snura, Dj Choka, Dk Cheni na wengine wengi.

Dk Cheni ambaye amekuwa karibu na Lulu kwa muda mrefu amesema huu ni wakati wa kumuombea Lulu kwa kuwa hakuna anayejua kesho atapata mkasa gani.

Katika mtandao wa Instagram aliweka picha ya Lulu na kuandika: "Tumuombee mtoto huyu kwa kuwa hakuna anayeijua kesho yake,".
Read More

Lulu Michael Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Miwili Jela

Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imemhukumu kwenda jela miaka miwili muigizaji wa filamu bongo Elizabeth Michael (Lulu) ambaye alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Jaji Sam Rumanyika aliyekuwa anaendesha kesi hiyo, na kusema kwamba mshtakiwa amekutwa na hatia ya kuua bila kukusudia kutokana na ushahidi wa mazingira, hivyo atatumikia kifungo cha miaka miwili jela.

"Ushahidi wa mazingira unaweza kutumika kama msingi pekee wa kumtia hatiani mshtakiwa tena mshtakiwa pekee, sasa ninapokwenda kuangalia maelezo ya mshtakiwa kama yanakidhi vigezo nilivyosema awali, kwa mujibu wa mshtakiwa alisema alianza kupigwa na marehemu, marehemu alilewa lakini kuhusu mshtakiwa anatakiwa kutoa maelezo yanayo jitosheleza, kwa hili mshtakiwa alijikanganya" amesema Jaji Rumanyika.

Jaji Rumanyika ameendelea kwa kusema kwamba.."mshtakiwa katika maelezo yake hakueleza kuwa marehemu alianguka au laah wakati anamkimbiza, maelezo ya Dkt. Josephine siyo maelezo ya cheti cha hospitali, hayakuwa na hadhi ya hospitali".

"Inakinzana na hekima ya kawaida kwamba hata pale marehemu alipoendelea kumpiga na kumshambulia na akaenda kiwango cha kumtishia kumuua, mstakiwa hakuthubutu hata kumpiga, ina maana alifanya kama maneno ya biblia yanavyosema mtu akikupiga shavu la kushoto mgeuzie na la kulia lakini hili mshtakiwa hakulisema.", amesema Jaji Rumanyika.

"Na wakati huo mshtakiwa alikuwa na miaka 17, leo ana miaka 22, alikuwa mtoto hivyo asingetambua kuwa kinachofanyika ni kibaya au kizuri, huyu mtoto sio mshtakiwa aliyelengwa nasheria ya watoto, kama mtoto wa umri huu na anaweza kafanya ya watu wazima,  mahakama hii haikubaliani bali mshtakiwa ni mkomavu, hakuna mashaka kuwa kifo cha marehemu kilitokana na ugomvi", ameendelea kusema Jaji Rumanyika mahakamani hapo.

Baada ya hapo jaji rumanyika aliwapa nafasi upande wa mshtakiwa kujitetea ambapo wakili wake Peter Kibatala alimtetea mshakiwa kwa kusema kuwa mshtakiwa anategemewa na familia yake.

Baada ya hapo Jaji Rumanyika alitoa hukumu yake na kumuamuru mshtakiwa kwenda jela kwa miaka miwili.

Elizabeth Michael (Lulu) anahukumiwa kwa kumuaa aliyekuwa mpenzi wake Steven Charles Kanumba ambaye pia ni muigizaji mwenzake, mnamo April 7, 2012.
Read More

Hatma ya Lulu kubaki uraiani au Gerezani Kujulikana Leo

Wadau wa sanaa ya filamu nchini masikio yao leo yatakuwa katika Mahakama Kuu ambako kutakuwa na tukio kubwa katika tasnia hiyo wakati itakapotolewa hukumu ya kesi inayomkabili mwigizaji maarufu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu.

Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua mpenzi wake Steven Kanumba bila kukusudia, kinyume cha kifungu cha 195 cha kanuni za adhabu (PC), Aprili 7, 2012, Sinza Vatican jijini Dar es Salaam kufuatia ugomvi wa kimapenzi ulioibuka baina yao.

Hapana shaka kuwa hii ni hukumu ambayo inasubiriwa kwa hamu na wadau wa sheria, sanaa ya uigizaji, wapenzi wa filamu, ndugu, jamaa na marafiki wa mshtakiwa huyo na wa marehemu Kanumba na hata jamii kwa jumla.

Hii inatokana na ukweli kwamba ni moja ya kesi zilizovuta hisia za makundi yote katika jamii tangu kutokea kwa tukio hilo, kushtakiwa kwa msanii huyo, jinsi jamii ilivyokuwa ikifuatilia mwenendo wa kesi pamoja na kuibua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya jamii na hata vijiweni.

Wakati upande wa mashtaka ukidai kuwa Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia, Lulu mwenyewe mara zote amekuwa akikana mashtaka hayo akidai kuwa hahusiki kwa vyovyote na kifo cha mpenzi wake huyo.

Hata hivyo, mvutano huo baina ya mshtakiwa huyo na upande wa mashtaka unatarajiwa kuhitimishwa leo na Jaji Sam Rumanyika aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo.

Kama ilivyo ada kwa kesi yoyote, kila upande yaani upande wa mashtaka na wa utetezi (mshtakiwa) utakuwa unatarajiwa moja kati ya mambo mawili; mshakiwa kutiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu au kuachiwa huru.

Hivyo ndivyo inavyotarajiwa kutokea pia kwa hukumu ya msanii huyo itakaposomwa na Jaji Rumanyika na kama mshtakiwa atatiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo au atabaki uraiani kuendelea na maisha kama kawaida, iwapo mahakama haitamtia hatiani.

Kwa vyovyote itakavyokuwa matokeo ya hukumu hiyo yatakuwa na uzito wa pekee kwa msanii huyo kwani ndiyo itakayotoa mustakabali wa maisha yake.

Hii ina maana kwamba iwapo apatikana na hatia, basi atakabiliwa na adhabu, jambo ambalo litabadili historia na mustakabali wa maisha yake kwa jumla, ingawa inategemeana na adhabu atakayopewa.

Lakini iwapo atashinda kesi hiyo, basi yeye ndiye atakayekuwa na furaha kubwa kwa kuwa atakuwa ameepuka adhabu, na hivyo kuendelea na maisha akiwa huru.

Kwa hiyo, wakati wa hukumu hiyo Jaji Rumanyika anatarajiwa ama kumtia hatiani na kumhukumu adhabu au kumwachia huru.

Katika kufanya hivyo, jaji huyo atazingatia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi wa pande zote, yaani upande wa mashtaka na upande wa utetezi pamoja na vielelezo mbalimbali.

Mbali na ushahidi huo na vielelezo vyake, pia Jaji Rumanyika atazingatia sheria zinazoongoza kesi za namna hiyo pamoja na uamuzi wa kesi mbalimbali zilizowahi kuamuliwa zenye mashtaka na hata mazingira yanayofafana nayo.

Katika kesi hasa za mauaji ama ya kukusudia au ya bila kukusudia huwa kuna ushahidi wa aina mbili. Mosi ni ushahidi wa moja kwa moja, yaani ushahidi wa kushuhudia tukio.

Pili, ni ushahidi wa kimazingira. Huu ni ushahidi ambao hakuna shahidi aliyeshuhudia moja kwa moja tukio likitokea, bali mshtakiwa huhusishwa na tukio kulingana na mazingira yaliyokuwapo kabla au wakati wa tukio husika.

Katika kesi ya Lulu, kwa mujibu wa Jaji Rumanyika, upande wa mashtaka umeegemea kwenye aina hii ya pili ya ushahidi wa mazingira, kwani kati ya mashahidi wanne wa upande huo hakuna hata mmoja aliyeshuhudia tukio hilo.

Ushahidi wa upande wa mashtaka unasema Kanumba alifariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo lijulikanalo kwa kitaalamu kama brain concussion, lililosababisha mfumo wa upumuaji kushindwa kufanya kazi baada ya kujibamiza ukutani upande wa kisogoni.

Hivyo upande wa mashtaka unadai kuwa mshtakiwa ndiye aliyesababisha Kanumba kujibamiza ukutani (ukimaanisha kuwa alimsukuma) na hivyo kupata tatizo lililosababisha kifo chake.

Hata hivyo, hakuna shahidi hata mmoja aliyeieleza mahakama kuwa alishudia mshtakiwa akifanya jambo ambalo lilisababisha kifo cha Kanumba, badala yake kuna ushahidi wa kusikia sauti za ugomvi baina ya Lulu na Kanumba chumbani mwa Kanumba.
Read More

Lulu Michael akutwa na hatia ya kuua bila kukusudia, hukumu yake kutolewa Novemba 13

Kesi inayomkabili muigizaji wa Filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo alhamisi imeendelea kusikilizwa Mahakamani ambapo washauri watatu wa Mahakama kuu wamesema mshitakiwa Lulu aliua bila ya kukusudia.

Baada ya kusikiliza maoni ya baraza la wazee leo Mahakama kuu ya tanzania, imesema Elizabeth Michael amekutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia, muigizaji mwenzake Steven Kanumba ambaye alikuwa mpenzi wake na hukumu yake itatolewa Novemba 13.

Wazee hao ambao walikuwa watatu, kila mmoja alitoa maoni yake na kusema kwamba muigizaji huyo ana hatia ya kuua bila kukusudia, kwani marehemu alikuwa na mwili mkubwa zaidi ya mshtakiwa.

Kabla ya  wazee kutoa maoni, Jaji Rumanyika ambaye ndiye anayeendesha kesi hiyo, alisoma maelezo ya ushahidi wa pande zote mbili na kusema kwamba ushahidi upande wa mashtaka umejikita katika ushahidi wa kimazingira kwa kuwa Lulu ndiye mtu wa mwisho kuwa na Kanumba, kisha kusikiliza maoni hayo.

Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Novemba 13, ambapo hukumu yake itasomwa.

Read More

DIAMOND Msamehe Baba'ko, Mbona Q-Chief Aliweza?


Ni kweli inauma mno kutelekezwa na mzazi. Mimi ambaye baba na mama yangu walinilea kwa umoja wao pamoja na umaskini wetu, huwa nawaza ingekuwaje baba au mama asingekuwa karibu yangu? Malezi ya mzazi mmoja au wote wasingekuwepo. Inaumiza sana!

Hiyo ndiyo sababu naweza kuhisi kile ambacho kinamuumiza mtoto aliyetelekezwa. Mimi ni baba, najua ni kiasi gani mtoto wangu ananihitaji kwa ukaribu. Upendo wangu kwake umekuwa zawadi yake muhimu kutoka kwangu kuliko kitu chochote. Hivyo basi, najua atapitia machungu kiasi gani kama nikimtelekeza.

Chukua hii; Kwa hali yoyote ile, mzazi hana leseni ya kumtelekeza mtoto wake. Changamoto zije na ziondoke, hakikisha unabaki umemganda mwanao. Kosa la kumtelekeza mtoto linafanana na la kuua. Huyo ni mtoto wako, unamkimbia, unataka alelewe na nani?

Mwanamuziki Aboubakar Shaban Katwila ‘Q Chilla’ katika nyimbo zake Aseme na Si Ulinizaa, alionesha wazi kuumizwa na alivyokataliwa na baba yake, Shaban Katwila, tangu akiwa mimba.

Baba mcheza soka maarufu Tanzania, mtoto anaishi kwa shida, akisaidiwa na wasamaria wema, wakati huo mama mzazi alishafariki dunia. Q Chilla akaokotwa! Ukitafakari vizuri unaweza kuhisi Q Chilla aliumia kiasi gani.

Baada ya vilio vingi, mzee Katwila alitumia njia mbalimbali kutengeneza suluhu na mwanaye. Wakasameheana na kudumisha upendo kama mtu na mzazi wake. Tangu hapo, Q Chilla alipitia vipindi vingi vibaya, baba yake akawa msaada wake.

Mara ya mwisho nilipozungumza na Q Chilla, alikiri kuwa yupo kwenye kipindi kizuri sana cha maelewano na baba yake na kwamba alikuwa mmoja wa watu waliompigania aweze kuacha matumizi ya dawa za kulevya baada ya kutopea.

Chukua hii; Watu hufanya makosa lakini ni haohao hugeuka watu wazuri. Anaweza kukutenda leo lakini kesho akakufaa. Ni mwongozo wa wahenga kuwa hupaswi kutupa jongoo na mti wake.

Isisahaulike migogoro ya kimapenzi husababisha maumivu mengi kwa watoto, vilevile uchonganishi kati ya mtoto na mzazi mmoja. Mama akibaki na mtoto baada ya kutofautiana na baba yake, anaweza kumjaza mtoto sumu kuwa baba yake alimsusa, hakumjali.

Hutokea kwa akina baba ambao hulea watoto bila mama zao, nao hutema sumu yenye uchonganishi kati ya mtoto na mama yake. Ni vizuri sana mtoto anapopevuka ayapime matukio ya nyuma kwa kutumia akili ya kikubwa. Anaweza kupata majibu ambayo ni mazuri mno kwa maisha yake.

Kwanza mzazi ambaye anamtelekeza mtoto wake ni mtu ambaye anastahili mno kuhurumiwa, maana hawezi kuwa sawasawa. Binadam aliyekamiliki kiakili anatambua kuwa mtoto ni sehemu ya maisha yake, hatathubutu kumtelekeza.

Stadi wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ ana machungu yake. Alishapata kueleza kuwa baba yake, Abdul Juma hakuwa na muda naye kipindi anakua, hivyo jukumu la malezi na ukuaji wake, lilisimamiwa na mama yake, Sanura Kassim ‘Sandra Khan’.

Malezi ya Diamond yalijaa machozi na jasho, mama yake akihangaika huku na huko kuhakikisha mtoto wake anapata mahitaji muhimu, japokuwa haikuwezekana kupata yote. Kwamba wakati huo wa mateso, baba yake aliendekeza utoto wa mjini, akashindwa kuzingatia kuwa yeye ni baba.

Diamond naye ameamua kutoa adhabu kali kwa baba yake. Hamshirikishi kwenye mafanikio yake. Wengi tu wanakula matunda ya kazi yake ya muziki ambayo imempa umaarufu mkubwa barani Afrika na kwingineko duniani, baba mtu haambulii chochote.

Baba Diamond anapigika, anaumwa anakosa mpaka msaada wa matibabu, wakati huo Diamond anatapanya fedha kwa watu wengine. Inawezekana anafanya hivyo kutokana na hasira kali alizonazo, ila zimezidi kipimo.

Leo hii Diamond hana ubavu wa kumfuta baba yake kwenye mzunguko wa maisha yake, isipokuwa atabaki kuwa baba yake anayemchukia. Na je, hizo chuki hazifiki mahali zikaisha?

Kuna adhabu kubwa ambayo Diamond anashindwa kuitumia, na yenyewe ni kuwa chanya kwa baba yake. Angekuwa anamjali na kumpa huduma nyingi muhimu, angekuwa anamsuta kwa vitendo, kwamba yeye alimtelekeza kisha anamhudumia.

Uamuzi wa Diamond kutomjali baba yake ni kisasi. Na ni mwendelezo wa damu mbaya ambayo mara nyingi huhama kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mwingine.

Leo hii Diamond ni baba, yupo vizuri na mwanaye kwa sababu hakuna mgogoro kati yake na mama wa mtoto wake ambaye pia anatarajia kumzalia mtoto wa pili. Mama ni raia wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, mtoto aliyepo ni wa kike, Latiffah, wanatarajia wa kiume.

Inaweza kutokea baadaye Diamond akagombana na Zari kisha akawa mbali na watoto wake kwa sababu ni wadogo. Mama akatumia nafasi yake kuwajaza sumu watoto wake kuwa baba yao aliwatelekeza. Nao wakikua wakamchukia baba yao. Diamond anatakiwa ayapime hayo.

Huu ni wakati mzuri mno kwa Diamond kukata mnyororo wa chuki kati yake na baba yake. Kutosikia kilio cha baba yake ambaye anaumwa ugonjwa mkubwa (kansa), ni roho ngumu mno. Ni roho ngumu mithili ya ile ya Jenerali Idd Amin Dada wa Uganda.

Diamond anayo nafasi ya kumhudumia baba yake kama ambavyo mtu anaweza kujitolea kwa ajili ya raia wengine wenye matatizo wanaomgusa. Kiusamaria wema tu. Ajitolee tu!

Namkumbusha kuwa alimnunulia gari aliyekuwa mkongwe wa muziki nchini, marehemu Marehemu Muhidin Maalim Gurumo, baba yake akiwa anaishi katikati ya dhiki kubwa. Vilevile amekuwa akinukuliwa kutoa misaada mbalimbali, baba yake anateseka. Misaada sharti ianze nyumbani.

Hiyo chuki mpaka lini Diamond? Mbona hujakana kutumia jina lake? Unaitwa Nasibu Abdul Juma, huyo Abdul Juma unamwacha anataabika kwa sababu ya visirani vya nyakati za giza. Tafadhali Diamond usiwe na roho ya Idd Amin, haikufai. Zipo baraka nyingi utaongezewa baada ya suluhu yako na baba yako.

Imeandikwa na Luqman Maloto
Read More

Davido Ampiku Diamond Kama Muimbaji Mwenye Followers Wengi Instagram (Afrika)


Msanii wa Nigeria, Davido amefanikiwa kufikisha follower milioni 2.9 kwenye mtandao wake wa Instagram na kuwa muimbaji wa kwanza Afrika kuwa na followers wengi zaidi kwenye mtandao huo.

Mpaka wiki iliyopita nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz mwenye follower 2.7 milioni kwenye mtandao huo lakini kwa sasa atashika nafasi ya pili.

Mpinzani wa karibu wa Davido, Wizkid ana followers milioni 2.5.

Waimbaji wengine wenye followers zaidi ya milioni moja ni:

Don Jazzy 2.2 milioni
Tiwa Savage 2.2 milioni
Vanessa Mdee 1.8 milioni
Alikiba 1.4 milioni
Yemi Alade 1.2 milioni
Read More

Picha/Video: Diamond Akusanya Kijiji Mombasa


Mkali wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz ameendelea kuonyesha umwamba wake nchini Kenya katika show iliyofanyika Mombasa Jumamosi hii na kuhudhuriwa na maelfu ya watu.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri Afrika pamoja na kimataifa, ameendelea kudhihirisha ukubwa wake baada ya show yake kuhudhuriwa maelfu wa mashabiki.

Kupitia instagram yake, Diamond aliandika “It’s 4:35 am now in East africa… am now going to sleep then right after waking up, will start posting my all Mombasa show Pictures…. thanks,”

Angalia video:
Read More

Alikiba Aelezea ‘King Kiba’ ilikotokea, Adai si Mtu wa Maringo


Alikiba ametoa ufafanuzi wa wapi #KingKiba ilitokea kiasi cha kuitumia katika sehemu nyingi.

Akiongea kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz kilichoruka Alhamis hii kupitia EATV, Kiba alisema ni mashabiki ndio waliombatiza.

“Wakati nimepumzika kwenye muziki kulikuwa kuna vitu vingi vinavyoendelea, kuna watu walikuwa wanaongea kwenye social media. Kuna watu walikuwa wananifikia sababu wanapajua nyumbani wakasema ‘au tuanzishe kampeni’ wakaanzisha mimi najua masihara,” alisema.

“Kiukweli walichokuwa wanacomplain, kwanini Ali hutoi nyimbo, uko wapi, kuna watu wakaanzisha Bring Back Our Alikiba. Ndio ikaanzia pale watu wakaanza kuniita King Kiba kwasababu hata kwenye show pale wakawa wananiita hivyo,” aliongeza.

“Nikaona sawa haina shida, kila kitu ikawa hashtag #KingKiba, lakini sikufikiria kujiita hivyo.”

Kwa upande mwingine muimbaji huyo wa Aje alisema kuwa kutomfollow mtu yeyote Instagram haimaanishi kuwa anaringa.“Nimeacha kufollow watu [Instagram] nikiwa na watu 50k,” alieleza.

“Nilikuwa nataka nione, nimekuja kwenye muziki, je nina fans wangapi watanifollow mimi nikiwa kama AliKiba na kuangalia kazi zangu. Nilikuwa nasikia watu wanasema naringa na nini, lakini nilisema kwamba nitawafollow watu baadaye.”
Read More
Powered by Blogger.

Hot

© Copyright KAHAMA 24