Tecno Phantom 6 Mpya Kuja Na Saizi Tofauti

MATANGAZO

MATANGAZO
Watumiaji wa smartphone au maarufu Simu-Janja ni watu makini sana linapokuja suala la ukubwa wa simu, mwenendo wa masoko kwa sasa unaonyesha wanunuaji wengi wa simu wanavutiwa sana simu zenye kioo kipana.
 
Lakini sio wapenzi wote wa simu wanatamani simu zenye kioo kipana, watumiaji wengine wanapenda simu zenye ukubwa wa wastani. Fununu zilizotapakaa ni kuwa TECNO wanakuletea simu mpya Phantom 6 ambayo pia itakuja na matoleo mengine kama Phantom 6 Plus na Phantom 6 mini.
Fununu hizi zinaweka wazi kwamba watengenezaji hawa wakubwa wa simu za mkononi wana mkakati kabambe wa kuwavutia watumiaji wakubwa wa simu kununua matoleo haya mapya yanayotarajiwa kutoka Septemba hii pindi TECNO Phantom 6 itakapazinduliwa.

HAKUNA SHAKA JUU YA UKUBWA WAKE
Jambo hili linatia moyo huku TECNO ikiwekwa bayana katika uvumi unaosambaa angalau kwa vidokezo na muonekano ambao unasemekana ni rasmi Tecno Phantom 6 itaboreshwa zaidi na wala haitopunguziwa sifa zake kuu. 
Nafikiri hili ni jambo la kufurahisha sana kwa sababu mara nyingi tumekuwa tukiona makampuni mengi ya simu yakiwauzia wateja wao simu zenye uwezo mdogo katika maduka yao makubwa wakitumia jina la makampuni yanayobamba kwa kuuza simu. Watumiaji wengi wa simu siku hizi wako makini sana na hawadanganyiki kirahisi.

PHANTOM 6 NA MATOLEO MAPYA YA TECNO YATAKUWA NI GUMZO?
Watengenezaji hawa wakubwa wa simu za TECNO wamekuwa wakipambana kuweka toleo lao bora kabisa kwenye mauzo kuanzia Phantom A+ mpaka Phantom Z au Z mini, Phantom 5 na sasa Phantom 6. Swali linalobaki ni je, phantom 6 itabadilisha mtazamo wa baadhi ya wananuaji wa simu?
 
Unadhani wpenzi wa Smartphones wataanza kuiona Phantom 6 kama moja ya toleo la kipekee kama inavyotarajiwa na wengi? Na inasemekana kuwa Phantom 6 ama 6 + itakamata soko kubwa kipindi hiki endapo toleo zitambulishwa kwa upekee kwa wakati muafaka.

Mbali na fununu zote hizi tunasubirri kuona toleo rasmi la Phantom 6 kuzinduliwa ifikapo Septemba.  Endapo unahitaji taarifa zaidi unaweza kutembelea mitandao ya kijamii ya Tecno kama ilivyoorodheshwa hapa chini.