Viongozi wa kitaifa,Wazungumzia maendeleo yaliyoachwa na Rais wa kwanza Z'bar

MATANGAZO

MATANGAZO
Viongozi wa Kitaifa kutoka Zanzibar na Tanzania Bara wamesema Watanzania wanaendelea kumkumbuka Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume kutokana na Maendeleo makubwa aliyoyafanya wakati wa Uongozi wake miaka minane na kufanikiwa kuacha historia isiyofutika kwa kufanikisha Mapinduzi ya Zanzibar na tukio la kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania April 26, mwaka 1964.

Viongozi hao wametoa kauli jhiyo jana kwa nyakati tofauti, muda mfupi baada ya kukamilika kwa shughuli ya kumbukumbu ya miaka 46 ya kifo cha Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume iliyofanyika katika ofisi kuu ya Chama cha Mapinduzi iliyopo Kisiwandui visiwani hapa.

Walisema yanayooneka hivi sasa Zanzibar yametokana na dira ya maendeleo iliyoachwa na Marehemu Abeid Amani Karume ya kuwaletea wananchi Maendeleo katika sekta mbalimbali kwa kuondosha matabaka na kufanikiwa kujenga umoja wa kitaifa pamoja na kuasisi Muungano ambao umevunja rekodi kwa kudumu zaidi ya miaka 50.

Kila ifikapo April 7 kila mwaka, Watanzania huadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Sheikh Abeid Amani Karume ambaye aliuwawa na Wapinga Maendeleo na kuacha simanzi na majonzi kwa wanaharakati wa ukombozi wa Bara la Afrika.