Dereva Taxi Jela Maisha Kwa Kulawiti Mtoto Ndani ya Gari

MATANGAZO

MATANGAZO
Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kifungo cha maisha jela, dereva taksi Ally Mzako (29) baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka mitano.

Mzako ambaye ni mkazi wa Kinondoni, anadaiwa kumbaka mtoto huyo ndani ya gari, wakati mama wa mtoto huyo alipomuacha katika gari hiyo na kwenda duka la kubadilishia fedha za kigeni.

Hakimu mkazi, Flora Haule amesema Mahakama imeridhishwa na ushahidi wa mashahidi sita wa  upande wa mashtaka dhidi ya mshtakiwa.

Mzako alifanya kosa hilo, Julai 19, 2014, eneo la Clock Tower, mtaa wa Samora.