Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts

Tazama live: Man city vs Man United leo april 7

Read More

Marekani yatangaza vikwazo dhidi ya Warusi 38 na makampuni ya Urusi

Ikulu ya Marekani, White House imetangaza vikwazo dhidi ya Warusi 38 na makampuni, ikisema Marekani inakabiliana na kile kinachoendelea ikiwa ni mbinu za Serikali ya Urusi  za “vitendo vya kuvuruga” demokrasia nchi za Magharibi na ulimwenguni kote.

Katika muhtasari alioutoa msemaji wa White House Sarah Huckabee Sanders Ijumaa amesema Marekani bado inataka kushirikiana naUrusi

“Pia, kile tunachotaka kukiona ni serikali ya Urusi ibadilishe mwenendo wake kikamilifu. Tunataka kuendelea kuwa na mazungumzo na kufanya kazi siku za usoni kwa kujenga mahusiano mazuri,” Sanders amesema.

Vikwazo hivyo vitawekwa dhidi ya makampuni saba ya Urusi – ikiwemo Oleg Deripaska, kampuni ya aluminium ambayo ni mshirika wa karibu na Rais Vladimir Putin- na makampuni mengine 12 ambayo wanayamiliki au kuyahodhi.

Pia maafisa 17 wa serikali ya Urusi, na kampuni ya kutengeneza silaha inayomilikiwa na serikali ya Urusi na kampuni zake tanzu, benki ya Urusi, pia zitalengwa na vikwazo hivyo.
Read More

Balozi Wilbroad Slaa Awasilisha Hati Zake Za Utambulisho Kwa Mfalme Wa Sweden

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Wilbroad Slaa jana akiwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mfalme Carl XVI Gustaf wa Sweden.

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Wilbroad Slaa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa ofisi ya Mfalme wa    Carl XVI Gustaf wa Sweden baada ya utambulisho
Read More

Rais wa Zamani Afrika Kusini Jacob Zuma Afikishwa Mahakamani

Aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amefikishwa mahakamani leo katika mji wa Durban ili kujibu mashtaka ya rushwa, udanganyifu na kujitajirisha kinyume cha sheria. 
Kesi hii inasikilizwa kwa mara ya kwanza na inahusu biashara ya zamani ya mauzo ya silaha tangu miaka ya 1990.

 Rais wa zamani wa Afrika Kusini anashutumiwa kupokea rushwa kutoka kwa Thomson CSF – jina la zamani la kampuni ya Thales – katika mpango wa mkataba wa mauzo ya silaha wenye thamani ya karibu Euro Bilioni 4 ulioafikiwa mnamo mwaka 1999.

Wakati huo, Jacob Zuma alikua makamu wa rais wa nchi ya Afrika Kusini. Anashutumiwa kuwa alipokea jumla ya euro milioni 50 kutoka kampuni ya Ufaransa ya Thales. Kwa upande mwingine, aliahidi kupitishia zabuni kampuni hiyo ya Thales.

Kwa jumla, Afrika Kusini iliamua kutumia zaidi ya dola bilioni 10 kurejelea upya silaha zake. Silaha ambazo nchi hiyo haikuweza kuzihitaji wakati huo na ambazo hazitumiwi leo. Lakini sababu kuu ni kwamba zaidi ya dola milioni 300 (hongo) zililipwa wakati wa mikataba hii.
Read More

Rais wa zamani wa Korea Kusini amehukumiwa miaka 24 jela

Rais wa zamani wa Korea Kusini  Park Geun-hye, amehukumiwa miaka 24 jela baada ya kukutwa na hatia katika matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha nchi kushuka kiuchumi.

Park Geun-hye aliondolewa madarakani mwaka jana baada ya kutuhumiwa kutumia vibaya wadhifa wake na kusababisha kuanguka kwa uchumi.

Rafiki yake Choi Soon-sil, anayehusishwa na kashfa hiyo, alihukumiwa wiki mbili zilizopita hadi miaka 20 jela kwa kupokea hongo iliyotolewa na makampuni ya Korea Kusini, ikiwa ni pamoja na makampuni yai Samsung na Lotte.

Katika mashtaka yake, mwendesha mashtaka alimshtaki rais wa zamani kuwa “alisababisha mgogoro wa kitaifa kwa kuacha mtu ambaye hajawahi kushiriki katika usimamizi wa umma kuongoza nchi”.
Read More

China na Urusi Zaungana Kuikabili Marekani

UONGOZI wa Jeshi la China umeahidi kuisaidia na kuiunga mkono Urusi kijeshi kukabiliana na mataifa ya Magharibi dhidi ya mzozo wa kidiplomasia, vikwazo vya kiuchumi na mazoezi ya kijeshi.

Ahadi hiyo imetolewa Waziri wa Ulinzi wa China, Wei Feng ambaye yuko Urusi kuhudhuria mkutano wa saba wa kimataifa wa usalama wa Moscow akiwa ameambata na ujumbe wa maofisa wa ngazi za juu wa jeshi.

Feng alisisitiza kwamba ziara yake imeratibiwa moja kwa moja na Rais wa China, Xi Jinping.

Alisema alikwenda Moscow akiwa na ujumbe maalumu kutoka kwa Jinping katika kipindi hiki ambacho mataifa yote mawili yanaboresha majeshi yao na ushawishi wao duniani licha ya wasiwasi wa Marekani.

“Naitembelea Urusi kama waziri mpya wa ulinzi wa China kuionyesha dunia maendeleo ya hali ya juu ya uhusiano wetu na dhamira imara ya majeshi yetu kuimarisha ushirikiano wa kimkakati,” alisema Wei wakati wa mkutano wake na Waziri wa Ulinzi wa Urusi, Sergey Shoigu.

“Pili, kuisaidia Urusi kuendesha mkutano wa kimataifa wa usalama wa Moscow ili kuwaonyesha Wamarekani uhusiano wa karibu wa majeshi ya China na Urusi hasa katika hali ya sasa.

“Tumekuja kuwaunga mkono katika harakati zenu na hali inayowakabili,” aliongeza.

“Upende wa China uko tayari kuzungumza na Urusi kuhusu wasiwasi na misimamo yetu ambavyo vinawiana dhidi ya matatizo ya kimataifa katika majukwaa ya kimataifa pia,” alisema.

Hali hiyo inakuja huku mataifa hayo mawili yakiingia katika mzozo na Marekani katika maeneo tofauti kuanzia kijeshi hadi kiuchumi.

Rais Vladimir Putin wa Urusi na Jinping wa China wanaongoza kile kinachohesabiwa kuwa majeshi yenye nguvu yanayoshika namba mbili na tatu duniani nyuma ya Marekani.

Wakati Marekani imeendelea kuongoza kwa kipindi kirefu ikiwaacha kwa mbali washindani wake linapokuja suala la kijeshi, Moscow na Beijing zinakuja juu haraka zikilenga kuondoa pengo hilo na kudhibiti ushawishi wa Marekani katika siasa za dunia.
Read More

Marekani yalalamika baada ya China kulipiza kisasi

Marekani imeutaja ushuru wa forodha uliowekwa na China kwenye bidhaa zake kama “sio haki”, baada ya China kuweka ushuru wa bidhaa 128 zenye thamani ya dola bilioni 3, zinazoingizwa na Marekani nchini humo.

Bidhaa, zilizowekewa ushuru na China, ni pamoja na matunda na nyama ya nguruwe, ikiwa ni hatua za karibuni zaidi za ulipizaji kisasi kufuatia Marekani kupandisha ushuru wa bidhaa za chuma cha pua na bati kutoka China.

Aidha, hatua hiyo ya China imekuja baada ya mvutano mkali kati ya nchi hizo kutokana na masuala ya kibiashara, ambapo hofu kubwa ilikuwa ni kutokea kwa vita ya kibiashara kati ya mataifa hayo yenye nguvu za kiuchumi duniani.

Serikali ya Rais Donald Trump imesema ushuru wake ulilenga bidhaa za chuma cha pua na bati zinazoingizwa nchini Marekani ambazo ilizichukulia kama tishio dhidi ya usalama wa taifa hilo.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Taro Kano akiwa mjini Tokyo ameelezea wasiwasi wake kwa kuhusiana na hatua hizo za kisasi kati ya Marekani na China, na kusema kwamba zinaweza kuwa na matokeo makubwa kiuchumi.
Read More

Real Madrid Yaichapa Juventus Bao 3-0

 Real Madrid Yachapa Juventus Bao 3-0
Klabu ya Real Madrid ya Hispania imeichapa Juventus ya Italia bao 3-0 katika Michuano ya Ligi ya Klabu Bingwa barani Ulaya usiku wa kuamkia leo.

Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa nyumbani wa Juventus, Allianz Stadium, mabao ya Madrid yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 3 na 64 huku Marcelo akifunga ukurasa wa mabao kunako dakika ya 72.

Mchezo huo wa raundi ya kwanza unaitengenezea mazingira mazuri Real Madrid kusonga mbele hatua ya nusu fainali endapo italinda matokeo yake katika mzunguko wa pili.

Mbali na Madrid, Klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani imepata ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Sevilla ya Hispania.

Sevilla wakiwa katika Uwanja wao wa nyumbani, Estadio R. Sanchez Pizjuan walifungwa magoli hayo na Thiago Alcantara dakika ya 68 na Jesus Navas aliyejifunga 37.

Bao la Sevilla lilifungwa na Pablo Sarabia dakika 31 ya mchezo huo.

JUVENTUS (4-2-3-1): Buffon 6; De Sciglio 5, Barzagli 5, Chiellini 6, Asamoah 5 (Mandzukic 69, 5); Khedira 6 (Cuadrado 75, 6), Bentancur 6.5; Costa 5 (Matuidi 69, 6), Dybala 4, Sandro 5; Higuain 6.

BOOKINGS: Bentancur, Dybala



OFF: Dybala 67

SUBS: Szczesny, Cuadrado, Marchisio, Rugani, Lichtsteiner.

MANAGER: Max Allegri

REAL MADRID (4-3-1-2): Navas 6.5; Carvajal 6.5, Ramos 7, Varane 6, Marcelo 7; Modric 7 (Kovacic 82), Casemiro 6.5, Kroos 7; Isco 8 (Asensio 75, 6); Benzema 6 (Vazquez 59, 6.5), Ronaldo 9.



GOALS: Ronaldo 3, 64, Marcelo 72.

BOOKINGS: Ramos, Kovacic.

SUBS: Casilla, Vallejo, Bale, Hernandez.

MANAGER: Zinedine Zidane

REF: Cuneyt Cakir (TUR).
Read More

Update: Watanzania Wenzetu Waliokuwa Wametekwa huko DRC Congo Wameokolewa

Madereva wa malori kutoka Tanzania waliokuwa wametekwa katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hatimaye wameokolewa na vikosi vya jeshi la nchi hiyo.

Waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo amezungumza na shirika la utangazaji la BBC na kusema wote wameokolewa   na wako salama

Taarifa iliyotolewa jana  na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilieleza kuwa watekaji hao ni kikundi cha waasi cha MaiMai ambao baada ya kuyateka magari 8 toka Tanzania , waliwashusha madereva na kuwapeleka porini na kisha kuteketeza kwa moto malori manne ambayo yote ni ya Bw. Dewji. 

Waasi hao walioa saa 24 kuanzia jana saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Kimarekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia.

Read More

Madereva kutoka Tanzania watekwa nchini DRC.


Serikali imepokea taarifa za kutekwa kwa malori 12 katika eneo la Namoyo Jimbo la Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jana tarehe 14 Septemba 2016. Kati ya malori hayo nane yanamilikiwa na mfanyabiashara wa Kitanzania, Bw. Azim Dewji na mengine yanamilikiwa na wafanyabiashara kutoka Kenya.

Kwa taarifa zilizopatikana watekaji ni kikundi cha waasi cha MaiMai ambao baada ya kuyateka magari hayo, waliwashusha madereva na kuwapeleka porini na kisha kuteketeza kwa moto malori manne ambayo yote ni ya Bw. Dewji. Waasi hao wametoa saa 24 kuanzia jana saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Kimarekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia. 


Wametishia kuwaua mateka hao endapo hawatalipwa kiasi hicho cha fedha wanachokitaka itakapofika saa 10 jioni leo. Katika tukio hilo, madereva wawili wa Kitanzania wamefanikiwa kutoroka ambao ndio waliosaidia kutoa taarifa rasmi kuhusu tukio hilo.

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeshachukua hatua za awali za kuwasiliana na Serikali ya DRC ili kuhakikisha kuwa madereva hao wanaachiwa haraka iwezekanavyo wakiwa salama kabisa.

Tukio hili ni la pili kutokea katika miaka ya hivi karibuni ambapo mwaka 2015 Mashekhe kutoka Tanzania walitekwa nchini DRC lakini kwa ushirikiano wa Serikali hizi mbili zilifanikisha mashekhe hao kuachiwa huru bila madhara yoyote.

Serikali ingependa kuushauri Umma wa Watanzania hususan wafanyabiashara kuomba taarifa ya hali ya usalama kwa maeneo yenye matatizo ya kiusalama kama Mashariki ya Congo hususan Kivu ya Kusini kabla ya kusafiri kwenda maeneo hayo.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dar es Salaam, 15 Septemba 2016.
Read More

Apple to lower App Store 'tax'

Apple logo on side of store

If you sell an app, subscription or other product through the App Store, Apple gets 30% of the money.
That's how its been since the App Store's inception seven years ago.
But soon Apple will for the first time lower its App Store commission on one condition: if an app can retain a subscriber for over a year, the revenue split will be 85/15.
The change will apply immediately to existing apps with users that are more than a year old - potentially providing an injection of extra revenue for many companies.
Spotify, for example, boasted of having 20 million subscribers this time last year.
For the sake of argument, if even just half of those subscribers are still paying members today, the change could potentially represent around $15m in extra subscription revenue for Spotify every month, and that's probably a conservative estimate.

'Terrific news'

As well as price, Apple will introduce another significant change to App Store subscriptions. Until now, only apps in certain categories - media and entertainment content - could charge subscription fees. Soon, any app will be able to offer such an option.
This is widely seen as a way for Apple to encourage high-end productivity apps onto its mobile operating system, iOS.
"This could be the change that makes the market for professional-calibre iPad apps possible," wrote John Gruber, a technology writer and long-time Apple watcher.
"I think this is terrific news both for developers and users."
The danger, of course, is by opening up subscriptions to every type of app, Apple risks creating a frustrating environment that's irritating for users who were accustomed to the simple model of paid or free apps.
Then again, subscriptions are surely more likely to encourage quality compared to one-off payments - the challenge for developers shifts from being convincing people to pay once, to convincing them to keep paying, again and again.

Search ads

The revenue split change is just one piece of Apple's plans for its store, which now has 1.5 million apps on offer - second only to Google's Play store.
It means discovery for apps seeking to gain new users can be difficult, with limited possibilities for promotion within the store other than becoming an Apple "featured app", a lucrative accolade that can make or break a new app.
Soon, ads will appear at the top of searches made in the App Store. They will, Apple says, be relevant to the search in question, and be clearly marked as being a paid-for position. Ads won't be shown to users who are under 13.
Location data is used to power some of the ads, but users can opt out of this, Apple said, and no user data is shared with the advertisers in question.

Developer's conference

The changes have been announced ahead of Apple's annual Worldwide Developers' Conference, or WWDC.
More announcements are on the way, but it's traditional for WWDC to be more about software improvements than new hardware.
Microsoft, Facebook and Google have already held their equivalent events, and at each, artificial intelligence was the main talking point. Will Apple offer the same?
There's rumblings in the Valley that Apple lags way behind the others when it comes to machine learning and AI technologies - presenting a problem which one prominent observer warned could see Apple become the "next Blackberry".
Such talk is premature, of course, when talking about the world's most valuable company. The changes to the App Store - outlined in Apple's words here - are about maintaining dominance of the market, not chasing it.
Read More

Kupatwa kwa "Leicester City" hii hapa!


Leicester yafungwa 4 kwa 1 zidi ya liverpool!

Read More

Hawa ni mastaa wa US waliodai wataihama nchi hiyo Donald Trump akishinda Urais


Orodha kubwa ya mastaa wa Marekani imeapa kuihama nchi hiyo iwapo Donald Trump atashinda uchaguzi na kuwa rais.

Iwapo mgombea huyo wa chama cha Republican akishinda, mastaa kama Jon Stewart, Cher, Barbra Streisand, Samuel L. Jackson, Chelsea Handler na Lena Dunham wamesema watahamia Canada au nchi zingine duniani, lakini sio kuwa chini ya uongozi wa bilionea huyo mwenye mdomo mchafu.

“If he were elected, I’m moving to Jupiter,” aliandika muimbaji mkongwe, Cher.

Kwa upande wake muigizaji mkombwe, Jackson alisema, “If that motherf- -ker becomes president, I will move my black ass to South Africa.”

Hata hivyo wapo mastaa ambao awali waliwahi kutoa ahadi kaka hizo wakazivunja pindi George W. Bush alipoingia White House mwaka 2000.
Read More

Matusi yavunja mkutano wa Obama na Rais wa Ufilipino


Rais wa Marekani Barack Obama amevunja mkutano wake na Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte,  baada ya  Rais huyo, kumwita Obama ‘Mwana wa Kahaba’

Obama awali alikuwa amesema kwamba angemuuliza kiongozi huyo maswali kuhusiana na mauaji ya kiholela ya watu wanaotuhumiwa kuhusika katika ulanguzi wa dawa za kulevya Ufilipino.

Lakini Bw Duterte, ambaye ameunga mkono mauaji hayo, alisema iwapo hilo lingefanyika: "Putang ina (mwana wa kahaba) nitakutusi katika mkutano huo."

Maafisa wa Obama wamesema badala yake kiongozi huyo sasa atakutana na Rais wa Korea Kusini.

Msemaji wa baraza la Taifa la Usalama Marekani Ned Price amewaambia wanahabari kwamba Obama atakutana na Park Geun-hye katika mkutano wa Mataifa ya Kusini Mashariki mwa bara Asia (Asean) mjini Laos, ambapo viongozi wamekusanyika kwa mkutano mkuu.

Obama, aliyetua Laos baada ya kuhudhuria mkutano wa G20 mjini Hangzhou, China, alitarajiwa kuuliza maswali kuhusu ukiukwaji wa haki za kibinadamu Ufilipino.

Lakini akiongea mjini Manila Jumatatu kabla ya kuondoka kuelekea Laos, Duterte alishutumu hilo na kusema ni "kukosa adabu" na akamtusi rais huyo wa Marekani. Aliongeza kwamba: "Tutagaragazana matopeni kama nguruwe iwapo utafanya hilo."

Kisha, alizungumzia kampeni ya kukabiliana na walanguzi wa dawa za kulevya ambapo washukiwa 2,400, wakijumuisha walanguzi na watumizi, wameuawa nchini Ufilipino tangu achukue mamlaka mwezi Juni.

"Kampeni dhidi ya dawa za kulevya itaendelea. Wengi watafariki, wengi watauawa hadi tuangamize mlanguzi wa mwisho na kumuondoa kutoka barabarani ... hadi mtengenezaji wa mwisho wa dawa hizi auawe, tutaendelea."

 Obama awali alidunisha matusi hayo na kusema aliwaomba maafisa wake kuchunguza iwapo huu ni wakati mwafaka wa kuwa na mashauriano ya kufana.

Baadaye, maafisa wake walivunjilia mbali mkutano huo.

Ziara ya mwisho ya Obama bara Asia akiwa kama rais imejaa vioja. Alipowasili Uchina, alijip kwenye mzozo wa itifaki kati ya maafisa wa Marekani na Uchina ambapo alikosa kuwekewa zulia jekundu.

Matusi

Hii si mara ya kwanza kwa Rais Duterte kutumia lugha chafu kuwarejelea viongozi mashuhuri.

Alimwita Papa Francis "mwana wa kahaba", waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Keryy "mwendawazimu" na majuzi alimweleza balozi wa Marekani nchini Ufilipino kama "mpenzi wa jinsia moja ambaye ni mwana wa kahaba".
Read More

Hali Ngumu ya Maisha, Afisa wa Polisi Ajiua Kwa Kujipiga Risasi Jomo Kenyatta (JKIA)

Afisa wa polisi Caudencia Wausi alimejiua kwa kujipiga risasi kichwani katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta (JKIA) muda mfupi baada ya kuchapisha ujumbe wa kuashiria kuwa na mahangaiko maishani.

Koplo Caudencia Wausi alitumia bastola yake aina ya Jericho kujifyatulia risasi kichwani ndani ya choo dakika 13 tu baada ya kuchapisha ujumbe katika mtandao wake wa Facebook.

"Maisha ni magumu unapoishi katika ulimwengu ambapo kila mtu anapanga kukufanyia maovu.. na utafanya nini wakati ambapo huwezi kuvumilia au hauna uwezo wa nguvu za kuwatia nguvu wapendwa wachache katika maisha yako.!? hauna lingine la kufanya ila... kwa hivi nisadie Mungu "aliandika kwenye Facebook.

Kwa mujibu wa mkubwa wake, Bi Wausi alikuwa amerudi kazini kutoka mapumzikoni kabla ya kujiua baada ya kujifungia chooni, JKIA.

Inadaiwa alijifungua mkanda wake wa polisi na kuuacha katika chumba cha Control Room pamoja na fimbo yake kabla ya kujifungia chooni.

"Tulisikia tu mlio wa risasi na baadaye tukampata juu ya choo huku bastola yake ikiwa mkononi, alikuwa tayari ameaga dunia "alisema kamanda wa polisi katika uwanja wa ndege Rono Bunei.

Bwana Bunei alisema kisa hiki kimeshtua wenzake kwasababu afisa huyo hakuwa na dalili za kusongwa na mawazo.

" Alikuwa anapiga gumzo na wenzake asubuhi na nilimuona mwenye furaha, hakuonyesha dalili zozote za kuwa na mahangaiko "alisema Bw Bunei na kuongeza kuwa uchunguzi umeanza kubaini kilichosababisha afisa huyo kujiua.
Read More

SAMAGOAL: Mbwana Samatta Aipeleka Timu ya Genk Hatua Nyingine Ligi ya Europa League

Mtanzania mshambuliaji wa Kimataifa, Mbwana Ally Samatta amepata nafasi ya kucheza hatua ya makundi ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League.

Hii ni baada ya klabu yake ya KRC Genk ya Ubelgiji kupata ushindi wa jumla ya mabao 4-2 dhidi ya wapinzani wao Lokomotiva Zagreb ya Croatia.

Genk walipata ushindi wa 2-0 mechi iliyochezwa jana jioni.

Klabu hizo mbili zilitoka sare 2-2 mechi ya mkondo wa kwanza.

Samatta alifungia klabu yake bao la kwanza dakika ya pili naye mwenzake Leon Bailey akafunga la pili muda mfupi baada ya mapumziko.
Read More

Rais Yoweri Museveni Kutawala Uganda Milele, Muswada wa Kubadili Katiba Kuwasilishwa leo

Leo Serikali ya Uganda itawasilisha muswada Bungeni unaotaka kubadilisha Katiba ili Rais Yoweri Museveni aweze kutawala milele.

Nini maoni yako juu ya hiki kinachotaka kufanyika?
Read More

Mugabe aagiza wanamichezo wa Zimbabwe walioshiriki Olimpiki wakamatwe?


Kuna habari imesambaa mtandaoni kuwa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi wa nchi hiyo Augustine Chihuri kuwakamata wachezaji wote wa timu iliyokwenda kushiriki michuano ya Olimpiki nchini Brazil.

Inasema Mugabe amechukua hatua hiyo baada ya kuumizwa na wachezaji hao kushindwa kupata hata medali moja kwenye mashindano hayo huku pesa iliyowekezwa kwenye timu ili kuiwakilisha nchi ingeweza kutumiwa kununulia dawa na kujenga shule.

“Jambo hili ni sawa na mwanaume asiyelijali kuoa wanawake watano, maana yake nini? Nitahakikisha tunagawana hasara, wote watailipa serikali bila kujali huku wakijua kuwa fedha zilizowapeleka huko zinatoka kwenye mifuko ya wananchi,” Mugabe anadaiwa kusema.

“Tumepoteza pesa za taifa kwa ajili ya hao panya tunaowaita wanamichezo. Kama hauko tayari kujitoa na kushinda japo medali ya shaba kama wenzetu wa Botswana walivyofanya, sasa kwanini ulienda kupoteza pesa zetu,” ameongeza.

Cha kuchekesha zaidi, Mugabe alidaiwa kusema, “kama tulihitaji watu kwenda Brazil kuimba wimbo wetu wa taifa na kupeperusha bendera, tungewaagiza warembo na vijana watanashati kutoka Chuo Kikuu cha Zimbabwe wakatuwakilishe.”

Zimbabwe ni miongoni mwa mataifa ambayo wanamichezo wake hawakufanikiwa kushinda medali ikiwa inawakilishwa na wanamichezo 31. Mchezaji ambaye alionekana kufanya vizuri ni yule aliyekamata nafasi ya nane.

Hata hivyo kuna uwezekano habari hii inaweza kuwa ni ya kutengenezwa (satire) kama nukuu mbalimbali za kuchekesha ambazo amekuwa akidaiwa kuzisema.
Read More

Rais Obama Achukizwa na Tabia ya Mwanae Malia Baada ya Kunaswa Akipuliza Bangi


Obama na Mwanae Malia
Hivi karibuni, Malia alionekana akivuta bangi kwenye tamasha moja maarufu.

Kwa mujibu wa tovuti ya RadarOnline, vitendo vya hivi karibuni vya Malia vimemsononesha sana Obama anayemaliza muda wake mwaka huu kama rais wa Marekani.

Awali, video ilisambaa mtandaoni ikimuonesha Malia Obama, 18, akionekana kuvuta bangi kwenye tamasha la Lollapalooza huko Chicago mwezi uliopita.

Kisha Malia alihudhuria kwenye party iliyopo kwenye kisiwa ambacho familia yake ipo mapumzikoni iliyofungwa na polisi. Malia alihitimu mwaka huu kwenye shule maalum ya Sidwell Friends ya Washington, DC, na anatarajiwa kujiunga na chuo kikuu cha Harvard mwaka 2017.
Read More

Mwenyekiti wa kampeni ya Trump ajiuzulu


Mwenyekiti ya kampeni ya mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amejiuzulu miezi miwili tu baada ya kushika usukani.
Alichukua nafasi hiyo kama mwenyekiti wa kampeni, baada ya meneja wa zamani Corey Lewandowski kufutwa kazi mwezi Juni.
Mtaalamu huyo wa masuala ya siasa wa umri wa miaka 67, amekuwa chini ya shinikizo kufuatia uhusiano wake na rais wa zamani wa Ukrain Viktor Yanukovych ambaye anaipendelea Urusi.
Lakini haijulikani ni kwa nini aliondoka kutoka kwa kundi hilo la kampeni lililofanyiwa mabadiliko wiki hii kwa kuongezwa meneja mpya pamoja na mkurugeni mkuu.
Bwana Manafort amekosolewa siku za hivi karibuni baada ya gazeti la New York times kuripoti kuwa serikali ya Ukrain ilifichua ahadi za kumlipa dola milioni 12 kwa kumfanyia kazi bwana Yanukovych.
Read More
Powered by Blogger.

Hot

© Copyright KAHAMA 24